Idara ya Watoto yatima, Watoto Walio kwenye mazingira magumu na  Wajane 

Idara ya watoto yatima, watoto walio na mazingira magumu, wajane iliundwa rasmi mwaka 2007. Kabla ya hapo, kazi iliyofanyika ndani ya idara, ilikuwa chini ya idara ya wanawake na watoto.

Idara imejikita zaidi kuunga mkono makundi yenye mazingira magumu katika jamii. Watoto yatima wanasaidiwa kwa njia mbalimbali, kwa mfano kwa kuwalipia ada za shule na kuwapa vifaa vya msingi vya shule kwa shule za sekondari, vituo vya mafunzo ya ufundi au vyuo vikuu. Mara nyingi watoto huishi na ndugu zao ambao wanawasaidia. Kwa watoto yatima wawili, huongezewa huduma za msingi, kama chakula, nguo na bidhaa za muhimu za usafi. Ikiwa hakuna waangalizi, tunatoa malazi kwa yatima.

Kwa bahati mbaya, bado kuna watoto wanaofanyiwa unyanyasaji nyumbani kwao, ndiyo maana tungali tunawasiliana na wazee wa kijiji katika mkoa wetu. Mtoto anaponyanyaswa na wazazi au waangalizi, tunajaribu kuingilia kati, kwa mfano kuwapeleka shule ya bweni huko Lutengano.

Pia, tunaandaa na kutoa msaada wa kisaikolojia kwa watoto walio na mazingira magumu na yatima, kwa kuwaleta pamoja na wataalamu kutoka hospitalini au serikalini.

Idara  inawasaidia watoto, wajane wa kike na wa kiume au waangalizi wakiwa na masuala ya kisheria. Matukio hayo yanaripotiwa kwa mashirika yasiyo ya kiserikali ambayo hutetea haki za watu walio katika mazingira magumu mahakamani.

Kipengele kingine muhimu katika kazi yetu ni kuwasaidia watunzaji kiuchumi. Tunaandaa semina, ambapo tunawafundisha kuanzisha miradi inayozalisha kipato, kama kufuga wanyama, kupanda miti ya parachichi au kufuga nyuki.

Pia tunaendesha miradi yetu ya kuzalisha kipato, ambayo inatuwezesha kuwasaidia watoto yatima na watoto walio na mazingira magumu na kazi yetu. Miongoni mwa mingine, tuna mradi wa kuku, baadhi ya miti ya parachichi na msitu wa ekari mbili.

Inatia moyo hasa tunapoona kwamba msaada wetu una matokeo chanja. Katika miaka iliyopita, tumeshuhudia taarifa nyingi za mafanikio. Kwa mfano, watoto tuliowasaidia sasa wamemaliza chuo kikuu na kupata kazi nzuri. wapo tayari kurudisha fadhira, kwa kuunga mkono kazi ya kuwasaidia watu walio na maisha magumu kifedha.


Dhamira kuu

Kuwasaidia watoto yatima, watoto walio katika mazingira magumu na wajane wa kike na wa kiume katika kanisa la Moravian eneo la jimbo la Kusini, ili waweze kuishi maisha mazuri na ya kujitegemea.

Malengo
  • Kuwasaidia watoto yatima na watoto walio na shida kwa kuwapa elimu ya sekondari, mafunzo ya ufundi na Chuo Kikuu

  • Kuwawezesha watoto yatima na watoto walio na shida kwa kuwafundisha shughuli za kuzalisha kipato

  • Kutoa msaada wa kijamii kwa watoto yatima na watoto walio na maisha magumu (OVC) kwa kuwashauri

  • Kuwapunguzia kazi waangalizi / watunzaji.

  • Kutetea haki za OVC

  • Kuongeza uelewa katika makanisa na jamii kuhusu mahitaji ya OVC
  • Kuimarisha maendeleo ya kitaasisi na kibinadamu katika Idara ya OVC

HISTORIA YA MSICHANA ALIYELELEWA ,KUSOMESHWA NA IDARA YETU
Mkuu wa Idara: Mch. Nikwisa Mwakamele
Mawasiliano


Kanisa la Moravian Tanzania - Jimbo la Kusini
Idara ya Watoto yatima, Watoto Walio na mazingira magumu na Wajane.

S.L.P. 32
Tukuyu
Tanzania

Barua Pepe:   nikukamele@yahoo.com
Simu:     +255 753 700985
Kiswahili