Idara ya Wanawake na Watoto

Idara ya Wanawake na Watoto ilianzishwa mwaka 1952, na kiongozi  wa kwanza Annette Mbapa Kabisa. Lengo kuu la idara lilikuwa kuimarisha mchango wa wanawake wanaoutoa kanisani, kwa sababu idadi ya wanawake waliokuwa wakihudhuria kanisani ilikuwa kubwa, lakini hawakuhusishwa kikamilifu kwenye nafasi za uongozi na kutoa maamuzi. Jambo hilo limefanikiwa sana, Sasa, kuna wachungaji wa kike zaidi ya 53 na wainjilisti wawili wanaofanya kazi katika jimbo la Kusini , lakini bado kunahitaji la idadi hiyo kuongezeka.

Zaidi ya hayo, idara ya wanawake pia inasaidia wanawake katika maisha yao ya kila siku. Tunafanya semina kuhusu mada mbalimbali, kama uwezo wa kimaendeleo, miradi ya kuzalisha kipato, ujasiriamali, uongozi, afya, kozi za Biblia na malezi ya watoto. Lengo ni kuwasaidia wanawake ili wawe huru zaidi. Idara pia inaendesha miradi yake ya kuzalisha mapato, kama upandaji wa misitu, kujenga maduka ya kufanyia biashara na mingine.


Pia tunaandaa mikutano ya maombi mara kwa mara, ambapo wanawake huja na kuombea matatizo yao ya kila siku na jamii nzima. Katika mikutano hii, tunakusanya pesa, ambazo hutumiwa kulipa ada za shule kwa wasichana walio na shida na kuwapa vifaa vya msingi vya shule. Pia tunatembelea mikutano mbalimbali kutoka mashirika mengine, kama vile Baraza la Kikristo Tanzania (CCT) au bodi ya kitaifa ya Kanisa  la Moravian nchini Tanzania (MCT).

Katika ngazi ya usharika, idara ya wanawake na watoto inasaidia makundi ya walio na maisha magumu, kama wajane, wagonjwa na wafungwa, kwa kuwapikia chakula na kuwapa msaada wa kiroho. Hii ni njia ya kuonesha upendo na kuhubiri neno la Mungu kwa matendo.


Pamoja Tunaweza - "Together we can"

Pamoja Tunaweza ni moja ya miradi yenye mafanikio zaidi ya idara ya wanawake na watoto. Ni kundi la wanawake wapatao 10 ambao hutengeneza mikoba, mablanketi, mabegi, midoli na vitu vingine vingi. Vitu vinauzwa, kwa mfano katika Maua Café Mbeya, nyumba ya wageni ya Mbutusyo na katika ofisi ya idara ya wanawake.

Wanawake wote wana mashine zao za kushonea, hivyo wanaweza kufanya kazi wakiwa nyumbani. Hiki ni chanzo muhimu cha kupata kipato, kinachowasaidia kujitegemea na kuhudumia familia zao.


Baadhi ya bidhaa zetu:
Uongozi

Mkuu wa Idara: Mch. Tupokigwe Mwamasangula

Msaidizi: Lucy Panja 



Mawasiliano


Kanisa la Moravian Tanzania - Jimbo la Kusini
Idara ya Wanawake na Watoto

S.L.P. 32
Tukuyu
Tanzania

Simu: +255 763162120
Kiswahili