Shule ya Sekondari ya Lutengano

Shule ya Sekondari Lutengano ni taasisi binafsi, inamilikiwa na Kanisa la Moravian Tanzania jimbo la Kusini. Shule ina mila ya kudumu. Ilianzishwa mwaka 1950 kama shule ya kati ya wasichana. Mwaka 1972 ilikuwa na shule ya msingi, hivyo shule ililenga hasa kuwasaidia watoto wenye ulemavu. Mwaka 1982 ilikuwa shule ya sekondari ambayo inajulikana hadi leo. Majengo mengi ni ya miaka ya 1980, lakini yalikarabatiwa tangu wakati huo, na jitihada mpya za ukarabati zitaanza mwezi Julai 2019.

Zamani shule ilipoanza, idadi ya wanafunzi ilikuwa kubwa, kutokana na ukweli kwamba ilikuwa moja ya shule ya sekondari binafsi pekee katika mkoa. Katikati ya miaka ya tisini, wanafunzi hadi 1300 walisoma elimu yao ya sekondari katika Sekondari ya Lutengano. Idadi ya wanafunzi ilibadilika kwa miaka mingi, sasa karibu wanafunzi 220 wanatembelea taasisi yetu.

Moja ya malengo makuu ni kuwapa wanafunzi wetu mafunzo yenye ubora wa hali ya juu. Hii ilisababisha wanafunzi wetu wa kidato cha sita kupata ufaulu wa juu zaidi wilayani Rungwe mwaka 2018.

Shule ya Sekondari ya Lutengano inatoa mafunzo katika ngazi zote, kutoka kidato cha kwanza hadi cha sita. Ni shule ya mchanganyiko ya bweni na kutwa tunafundisha mikondo ifuatayo:

  • Sanaa 
  • Mkondo wa sayansi 
  • Masomo ya biashara
  • Kemia, biolojia na jiografia (CBG

Wafanyakazi

Shule ya Sekondari ya Lutengano imeajiri jumla ya walimu 22 na wafanyakazi 14 wasio walimu. Utawala wa shule una watu wafuatayo.

Mkuu wa shuleRev. Israel A. Kabuka
Makamu mkuu wa shuleLaurian James Majengo
Mtaaluma mkuuFaustine Hance Mwasakanyama
Msimamizi wa chakula na kantiniKaisa Asilia

Matroni

Atulea Kiando
Msimamizi mkuu wa marekebisho na ukarabatiJoram Jericho
Mkuu wa miradiRichard Anyingisye
Mhasibu wa shuleNdimwabuke Msyani

Idara

  • Idara ya lugha (Kiswahili na Kiingereza)
  • Idara ya historia
  • Idara ya uchumi
  • Idara ya hesabu
  • Idara ya TEHAMA
  • Idara ya jiografia
  • Idara ya biolojia
  • Idara ya fizikia na kemia

Vifaa

Vifaa vyetu vya shule vinasaidia na kuwezesha mchakato wa kujifunza kwa wanafunzi wetu na kuwapa urahisi katika maisha yao ya shule. Yapo mabweni makubwa, moja kwa wavulana na jingine kwa wasichana. Uwezo wa jumla wa mabweni ni wanafunzi 900. Kwa sasa, wanafunzi wapatao 160 wanakaa bwenini. Pia kuna maabara ya biolojia, maabara ya kemia na chumba cha kompyuta chenye kompyuta zipatazo 20 na projekta. Ukumbi wetu mkubwa wa chakula pia unaweza kutumika kuandaa matukio ambayo yanahitaji nafasi kubwa. Ukarabati wa maktaba ya shule unatarajiwa kukamilika mwezi Oktoba 2019.

Motto wa Shule

Hakuna elimu, bila nidhamu

Misingi ya shule

Upendo, Amani, Umoja, Uadilifu, Uwazi, Uaminifu

Lengo la shule

Kuwa kati ya shule bora katika mkoa.


Mawasiliano


Shule ya Sekondari ya Lutengano
S.L.P. 282
Tukuyu
Tanzania

Barua Pepe Shule:   lutenganosecondary@gmail.com 
Barua Pepe Mkuu:  israelkabuka@yahoo.com
Simu:          +255 767 674744
Kiswahili