Shule ya Sekondari ya Lutengano
Shule ya
Sekondari Lutengano ni taasisi binafsi, inamilikiwa na Kanisa la Moravian
Tanzania jimbo la Kusini. Shule
ina mila ya kudumu. Ilianzishwa mwaka 1950 kama shule ya kati ya wasichana.
Mwaka 1972 ilikuwa na shule ya msingi, hivyo shule ililenga hasa kuwasaidia
watoto wenye ulemavu. Mwaka 1982 ilikuwa shule ya sekondari ambayo inajulikana
hadi leo. Majengo mengi ni ya miaka ya 1980, lakini yalikarabatiwa tangu wakati huo, na jitihada mpya
za ukarabati zitaanza mwezi Julai 2019.
Zamani shule
ilipoanza, idadi ya wanafunzi ilikuwa kubwa, kutokana na ukweli kwamba ilikuwa
moja ya shule ya sekondari binafsi pekee katika mkoa. Katikati ya miaka ya
tisini, wanafunzi hadi 1300 walisoma elimu yao ya sekondari katika Sekondari ya
Lutengano. Idadi ya wanafunzi ilibadilika kwa miaka mingi, sasa karibu
wanafunzi 220 wanatembelea taasisi yetu.
Moja ya
malengo makuu ni kuwapa wanafunzi wetu mafunzo yenye ubora wa hali ya juu. Hii
ilisababisha wanafunzi wetu wa kidato cha sita kupata ufaulu wa juu zaidi
wilayani Rungwe mwaka 2018.
Shule ya Sekondari ya Lutengano inatoa mafunzo katika ngazi zote, kutoka kidato cha kwanza hadi cha sita. Ni shule ya mchanganyiko ya bweni na kutwa tunafundisha mikondo ifuatayo:
- Sanaa
- Mkondo wa sayansi
- Masomo ya biashara
- Kemia, biolojia na jiografia (CBG
Wafanyakazi
Shule ya
Sekondari ya Lutengano imeajiri jumla ya walimu 22 na wafanyakazi 14 wasio
walimu. Utawala wa shule una watu wafuatayo.
Mkuu wa shule | Rev.
Israel A. Kabuka |
Makamu mkuu wa shule | Laurian
James Majengo |
Mtaaluma mkuu | Faustine
Hance Mwasakanyama |
Msimamizi wa chakula na kantini | Kaisa
Asilia |
Matroni | Atulea
Kiando |
Msimamizi mkuu wa marekebisho na ukarabati | Joram Jericho |
Mkuu wa miradi | Richard
Anyingisye |
Mhasibu wa shule | Ndimwabuke
Msyani |
Idara
- Idara ya lugha (Kiswahili na Kiingereza)
- Idara ya historia
- Idara ya uchumi
- Idara ya hesabu
- Idara ya TEHAMA
- Idara ya jiografia
- Idara ya biolojia
- Idara ya fizikia na kemia
Vifaa
Vifaa vyetu
vya shule vinasaidia na kuwezesha mchakato wa kujifunza kwa wanafunzi wetu na
kuwapa urahisi katika maisha yao ya shule. Yapo mabweni makubwa, moja kwa
wavulana na jingine kwa wasichana. Uwezo wa jumla wa mabweni ni wanafunzi 900.
Kwa sasa, wanafunzi wapatao 160 wanakaa bwenini. Pia kuna maabara ya biolojia, maabara ya kemia na
chumba cha kompyuta chenye kompyuta zipatazo 20 na projekta. Ukumbi wetu mkubwa
wa chakula pia unaweza kutumika kuandaa matukio ambayo yanahitaji nafasi kubwa.
Ukarabati wa maktaba ya shule unatarajiwa kukamilika mwezi Oktoba 2019.
Hakuna elimu, bila nidhamu
Misingi ya shule
Upendo, Amani, Umoja, Uadilifu, Uwazi, Uaminifu
Lengo la shule
Kuwa kati ya shule bora katika mkoa.
Mawasiliano
Shule ya Sekondari ya Lutengano
S.L.P. 282
Tukuyu
Tanzania
Barua Pepe Shule: lutenganosecondary@gmail.com
Barua Pepe Mkuu: israelkabuka@yahoo.com
Simu: +255 767 674744