Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Rungwe Moravian

Chuo cha Rungwe VTC kilianzishwa na wamisionari mwaka 1903, ambacho ni chuo cha zamani zaidi cha mafunzo ya ufundi nchini Tanzania. Hapo mwanzo, hesabu rahisi na ujuzi wa vitendo wa namna ya kujenga nyumba ulifundishwa. Hata hivyo, kwa miaka mingi, masomo ya msingi zaidi na masomo ya ziada yaliongezwa. Chuo kilisajiliwa rasmi na serikali ya Tanzania mwaka 1976, na kupata namba ya usajili 00057. Chuo cha Rungwe VTC kinafanya Mitihani ya Taifa ya Msingi (National Based Exams) na Tathmini ya Msingi ya Uwezo (Competence Based Assessments). Kwa kuzingatia ukweli, kwamba  chuo cha Rungwe VTC kimekuwa kwa zaidi ya miaka 100, hatuna budi kusema kwamba chuo kimekuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya mkoa na Tanzania kwa ujumla, na tutaendelea kufanya hivyo. Chuo hasa kinahamasisha na kuwasaidia watoto yatima kupata elimu ya mafunzo ya ufundi, na wahitimu wote hupewa vifaa muhimu, vinavyowawezesha kuanza biashara zao wenyewe.


Chuo cha Rungwe VTC kinatoa kozi zifuatazo:

  • Ufundi wa magari
  • Ufundi umeme wa majumbani
  • Ushonaji na ubunifu wa mavazi
  • Useremala na uundaji
  • Ufundi Umeme wa Jua (Solar Electrical Installation)
Kozi hizi hukamilika kwa miaka miwili. Miongoni mwa masomo yanayofundishwa:
  • Sayansi ya Uhandisi

  • Hisabati

  • Mafunzo ya Kompyuta

  • Ubunifu wa michoro

  • Kiingereza

  • Ujuzi wa Mawasiliano

  • Ujuzi wa maisha

  • Ujasiriamali

Mpaka sasa Chuo hiki kinapokea Wanafunzi kutoka sehemu mbalimbali wanaojiunga na chuo hiki.


Vifaa

Mara kwa mara tunaboresha miundombinu yetu kwa ajili ya mazingira bora ya kujifunzia. Hata hivyo, kuna vifaa ambavyo tunatoa. Kuna karakana kwa ajili ya wanafunzi wetu wa useremala, darasa lenye mashine za kushonea, chumba cha kompyuta, karakana ya ufundi wa magari na mabweni mawili. Chuo kinatoa malazi, bweni la wasichana wanafunzi 60 na la wavulana wanafunzi 40.

PAKUA HAPA FOMU YA KUJIUNGA NA CHUO HIKI   >>>  FOMU YA KUJIUNGA NA CHUO.docx

Wafanyakazi

Chuo cha Rungwe VTC kimeajiri walimu 14 ambao hutoa mafunzo ya masomo mbali mbali, na baadhi ya wafanyakazi wengine wasio walimu. Utawala una watu wafuatayo:

Gwantwa J. Mwandoloma - Mkuu wa Chuo 





Mkuu wa Chuo
Gwantwa J. Mwandolomajgwantwa@gmail.com
+255621448990 / +255766609807
Mratibu wa Mafunzo


Karani/ KeshiaUpendo J. Kayunikayunipendo47@gmail.com
+255682409114/+255626505394


Mawasiliano

Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Rungwe Moravian

S.L.P. 32
Tukuyu
Tanzania

Simu: +255 621-448 990
             mail : jgwantwa@gmail.com


Kiswahili