Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Songea Moravian

Chuo cha Moravian cha Mafunzo ya Ufundi Songea kilianzishwa mwaka 2014 na Kanisa la Moravian Tanzania – jimbo la Kusini, kwa msaada wa Daktari Fritz Wolfgang na HMH (Herrenhuter Missionshilfe). Nambari ya hati ya usajili ni VET / RVM / PR / 2014 / C / 057. Chuo cha Songea VTC kinatoa kozi zifuatazo:

Kozi za muda mrefu (miaka 2):
  • Ufungaji wa umeme wa majumbani
  • Ushonaji
Kozi za muda mfupi:
  • Useremala na uundaji (kati ya miezi 3 na mwaka 1)
  • Mafunzo ya kompyuta (kati ya wiki 2 na miezi 6)
  • Ufungaji wa umeme wa majumbani (kati ya miezi 3 na mwaka 1)
  • Ushonaji (kati ya miezi 3 na mwaka 1)
Hivi sasa, karakana ya ufundi wa magari inaendelea kujengwa na inatarajiwa kukamilika mwishoni mwa 2019. Kuanzia mwaka 2020, chuo hicho kitatoa mafunzo ya ufundi wa magari.

Kwa sasa, wanafunzi 45 wamejiunga na kozi za muda mdefu chuoni kwetu. Ikiwa una nia ya kujiunga na chuo cha Songea Moravian VTC, unaweza kupakua fomu yetu ya kujiunga hapa:Ikiwa una nia ya kujiunga na moja ya kozi zetu fupi unaweza kuangalia gharama na muda wa kozi hizo katika nyaraka zifuatazo:

Vifaa

Tunatoa vifaa mbalimbali kwa wanafunzi wetu ili viwasaidie kufikia malengo yao. Kuna chumba cha kompyuta chenye intaneti, karakana ya ufundi wa umeme wa majumbani, na kozi za ushonaji, pamoja na karakana ya useremala.

Wafanyakazi

Hivi sasa, walimu saba wanatoa mafunzo katika chuo chetu na wafanyakazi wanne wasio walimu wanatusaidia.

MkuuMratibu wa Mafunzo
Gwantwa John Mwandoloma
Conrad Kayombo

Lengo

Kuwa na ufanisi na nidhamu, kwa lengo la kuwaendeleza vijana wa Tanzania.

Mtazamo

Kuwaelimisha na kuwafunza wanafunzi, ili waweze kushindana katika soko la ajira na kujiajiri.


Mawasiliano


Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Songea Moravian

S.L.P. 222
Songea
Tanzania

Simu:     +255 766 609 807
Barua Pepe:   songeamoravianvtc@gmail.com 
Web: www.songeamoravian-vtc.simplesite.com

Kiswahili