Hospitali ya Isoko

Hospitali ya Isoko, ni Hospitali teule ya wilaya ya Ileje tangu 1976, inamilikiwa na Kanisa la Moravian Tanzania – Jimbo la Kusini. Ilijengwa na Kanisa la Moravian jimbo la Kusini mwa Tanganyika kwa msaada kutoka Kanisa la Moravian Ulaya. Hospitali ilianza kama zahati miaka ya 1950 na ikawa Hospitali mwaka 1961. Ilianza na vitanda 50 na baadaye ilipanuliwa mwaka 1976 ikawa na vitanda 110. Siku hizi, Hospitali ina vitanda 122 na huajiri jumla ya watu wapatao 90. Hospitali ilisaini mkataba wa huduma na wilaya ya Ileje mwaka 2012.

Hospitali inapatikana kijiji cha Isoko, kata ya Kafule, tarafa ya Bundali, wilaya ya Ileje katika mkoa wa Mbeya. Hospitali iko pembezoni mwa mlima Kashima, ambao ni mlima mrefu zaidi katika wilaya. Mlima umezungukwa na uoto wa asili, ambao una mazingira mazuri na tulivu katika kijiji cha Isoko kwa mwaka mzima.

Hospitali ya Isoko iko umbali wa kilomita 200 kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mbeya na Hospitali ya kanda, kilomita 65 kutoka Hospitali ya Itumba na makao makuu ya wilaya na kilomita 65 kutoka makao makuu ya wilaya ya Rungwe.

Usimamizi

Daktari mkuuDr. Mashaka Shibanda
Katibu wa afya
Mr. Zacharia Kangele
Muuguzi mkuuMs. Asha Konki
Katibu msaidizi wa afya
Mr. S. Mlwafu
Mfamasia
Mr. Joseph Kajange
MhasibuMr. Norbert Dickson


Muundo wa shirika


Muundo wa shirika

Surgical DepartmentOperating Theatre, male- and female Surgical Ward
Internal MedicineMale- and female medical ward
PaediatricPaediatric ward
Obstetrics and GynaecologyLabour room

Antenatal ward

Postnatal ward

Neonatal ward
PharmacyDispensing

Pharmacy store
Radiology
Ultra sound

X-Ray
LaboratoryClinical laboratory

Mortuary
AdministrationMedical record

Registry

Accounting

General Store (procurement)

Workshop (Medical engineering)

Workshop (others)
OrthopaedicOrthopaedic

Physiotherapy
PsychiatricPsychiatric
PharmacyDispensing

Pharmacy store
RadiologyUltra sound

X-Ray

Idadi ya wagonjwa

Jedwali lifuatalo linaonyesha kazi ya Hospitali ya Isoko kati ya mwaka 2010 na mwaka 2014.

 

DESCRIPTION

2010

2011

2012

2013

2014

Mahudhurio ya wagonjwa wa nje (OPD)

19,743

20,431

22,942

14,882

10,417

Mahudhurio ya afya ya uzazi wa mtoto

    434

516

643

 

5,881

Mahudhurio ya watoto chini ya miaka mitanomitano

9,598

2,024

939

7,231

988

Kliniki ya wajawazito

    878

1,339

989

586

740

Family planning

    2,015

1,758

2,032

2,383

1,078

Wastani wa wagonjwa wa nje kila siku

50-60

60

60

51

29

Idadi ya wagonjwa waliolazwa

 5,355

3,297

4,303

3,874

3,914

Waliojifungua

725

52

632

579

801

Upasuaji mkubwa

180

202

211

383

183

Upasuaji mdogo

360

422

344

394

240

Uchunguzi wa kimaabara

14,113

11,189

13,028

13,244

17,299

X –ray zilizochukuliwa

831

706

764

640

357

Kitengo cha meno

37

316

541

754

796



Mtazamo

Kuwa watoa huduma bora wa afya zenye ubora na gharama nafuu, kwa kuzingatia maadili ya kibinadamu.

Mission

Provide quality, affordable and accessible health care services to all the people in the area with high professional care for social economic sustainability.

Lengo

Kutoa huduma bora za afya, bei nafuu na zinazopatikana kwa watu wote katika eneo hilo na huduma ya juu ya kitaaluma kwa ustawi wa kiuchumi wa jamii.

Maadili

Upendo - Tunasisitiza upendo wa kindugu kati ya watu.

Uadilifu - Nidhamu ya juu katika kukamilisha kazi.

Uaminifu - Kama kituo cha kanisa tuna uaminifu mkubwa kwa jamii yetu.

Utawala Bora - Tunatoa huduma zetu kwa kuzingatia kanuni za utawala bora.


Miradi Yetu

Mradi wa Watoto yatima - Mpango wa kituo cha watoto yatima Isoko ulianza mwaka 1996, baada ya kusaini makubaliano kati ya Dinari ya Berg Strass - Mitte nchini Ujerumani na Kanisa la Moravian Tanzania – Jimbo la Kusini.
Malengo makuu ya mradi ni kuwasaidia watoto yatima kwa mahitaji kama nguo, matandiko, ada ya shule na huduma za matibabu. Kati ya mwaka 2012 na mwaka 2014, wastani kwa mwaka watoto yatima wapatao 171 walisaidiwa.

Bustani ya dawa za asili

Mradi wa Artemisia - Mradi wa dawa za asili wa mmea artemisia ulianzishwa na Mission 21 tangu mwaka 2008. Inahudumia watu vijijini, maeneo ya mbali ya MCT-SP. Mradi unalenga kupunguza magonjwa yaliyopo katika jamii. Mmea mkuu ni Artemisia, ambao unaimarisha kinga za mwili dhidi ya malaria kwa njia ya asili.



Shughuli za kuongeza kipato

Msitu - Hospitali inamiliki hekta 40 za msitu zenye misonobari 46,502 katika kijiji cha Nachibughubughu-Mbangala. Ni moja ya misitu bora zaidi na iliyopandwa sana katika wilaya.

Msitu

Nyumba ya mapumziko - Hospitali hutumia jengo moja kama nyumba ya mapumziko. Ina vyumba sita na ukumbi mdogo. Ni nyumba ya thamani, ambayo viongozi wengi wa serikali huitumia kwa kulala na kufanya mikutano, semina na warsha.

Mgahawa - Hospitali inamiliki mgahawa mdogo. Wateja wake ni wafanyakazi wa hospitali, ndugu wa wagonjwa na wageni wa hospitali. Kwa sasa, hospitali huhudumia chakula cha asubuhi na cha mchana.

Karakana ya useremala – Karakana ya useremala iko katika eneo la hospitali. Karakana hiyo ina vifaa na mashine za kukatia. Karakana inawezesha utekelezaji wa shughuli za hospitali kama vile ukarabati na urekebishaji wa majengo ya hospitali.

Mashine za kuchongea na kukatia - Mashine hufanya kazi na umeme. Wakati wa kiangazi mashine hazifanyi kazi kutokana na uzalishaji mdogo wa nishati wa maji.

Nyumba ya wauguzi wa wagonjwa - Nyumba ya wauguzi ina hosteli mbili, moja kwa wanawake na nyingine kwa wanaume. Pia kuna jiko, ambalo wauguzi hutumia kuandaa chakula cha wagonjwa.


Mawasiliano

Hospitali ya Isoko

S.L.P. 1
Isoko-Ileje
Tanzania

Barua Pepe: isokohospital6@gmail.com
Simu:
Daktari mkuu +255 754 915622
Katibu wa afya  +255 755 052726

Kiswahili