Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Nambumbo Moravian

Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Namtumbo kilianzishwa mwaka 2016 na Kanisa la Moravian  Tanzania – jimbo la Kusini, kwa msaada wa HMH (Herrnhuter Missionshilfe). Tunakaribisha wanafunzi wa aina zote bila kujali utofauti wa kiuchumi na wa kidini, lengo kuleta maendeleo katika jamii.

Tunatoa kozi zifuatazo:

Kozi za muda mrefu (miaka 2):

  • Ufundi wa umeme wa majumbani
  • Ushonaji

Kozi za muda mfupi (miezi 3 hadi mwaka 1)

  • Ufundi wa umeme wa majumbani
  • Ushonaji 
  • Mafunzo ya kompyuta
Kwa sasa, wanafunzi 35 wamejiunga na kozi zetu za muda mrefu. Pia, tuna mpango wa kutoa kozi ya ufundi wa magari, kuanzia mwaka 2020. Ukipenda kujiunga na chuo cha Nambumbo VTC, unaweza kupakua fomu yetu ya kujiunga hapa.

Nambari ya hati ya usajili wa chuo ni VET / RVM / PR / 2018 / C / 091.

Vifaa

Tunatoa vifaa mbalimbali vyenye lengo la kuwahakikishia  wanafunzi wetu mazingira mazuri ya kujifunzia. Chuo kina chumba cha kompyuta chenye kompyuta 9 na karakana yenye mashine za kushonea kwa wanafunzi wa ushonaji. Pia kuna mabweni kwa wavulana na wasichana yenye miundombinu ya kisasa, kila bweni lina nafasi kwa wanafunzi 16. Zaidi ya hayo, karakana ya magari inajengwa, kwa ajili ya kutoa kozi ya ufundi wa magari, ambayo itaanza mwaka 2020.

Wafanyakazi

Hivi sasa, walimu watano na mlinzi mmoja wanafanya kazi katika chuo cha Mafunzo ya Ufundi Namtumbo.

MkuuMakamu Mkuu
Barnaba Mulundi
Gibson Mwamahonje


Kauli mbiu ya Shule

Kama unaona ufundi ni ujinga, jaribua kuwa mjinga.

"If you are being told that vocational training education is ignorant, try to be ignorant."




Mawasiliano

Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Nambumbo Moravian

S.L.P. 77
Namtumbo - Ruvuma
Tanzania

Simu:     +255 764 194737
Barua Pepe:   namtumbomoravianvtc@gmail.com

Kiswahili